0
Kocha wa Simba, Goran Kopunovic amesema mambo yatabadilika na kikosi chake kufanya kazi kwa uhakika lakini muda bado unahitajika.

Kopunovic amesema bado Simba ina kikosi bora kuliko wengi wanavyofikiria.
“Kweli tumepoteza mchezo dhidi ya Stand. Hii inatokea, kweli kutokuwa makini au kukosea ni chanzo cha kutofanya vizuri.
“Lakini kuna mambo ya kufanya, bado tunaendelea kubadilisha. Bado tunapambana, huenda Simba wanatapwa kuwa wavumilivu.
“Sijui kabla, lakini kwa kipindi changu, mimi naona hatujapita sehemu ndefu ambayo utasema tumeharibu sana.
“Lakini hatuwezi kuendelea au kusubiri tuharibu tu. Tunapambana na mambo yatakwenda vizuri kikubwa waamini tunapambana na tutaendelea kubadilisha mambo kadhaa,” alisema Kopunovic.
Simba nayo imekuwa na makosa mawili, moja kutotengeneza nafasi nyingi za kufunga. Lakini zinapopatikana, haiko makini kuzitumia.

Post a Comment

AddThis

 
Top