0
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amethibitisha kuwa mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo, Didier Drogba anarudi darajani.

Nyota huyo raia Ivory Coast  aliitumikia Chelsea kwa miaka 8 na kuondoka mwaka 2012  ambapo alijiunga  Galatasaray ya  Uturuki baada ya kutwaa kombe la UEFA dhidi ya Bayern Munich.
Ingawa ana miaka 36 kwasasa, Mourinho anaamini bado anaweza wa kucheza ligi kuu nchini England na michuano ya kimataifa.

Post a Comment

AddThis

 
Top