0
Waamuzi wa mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 kati ya Tanzania (Serengeti Boys) na Afrika Kusini (Amajimbos) wanawasili leo (Julai 15 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.

 Mechi hiyo itafanyika Ijumaa (Julai 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam na itachezeshwa na waamuzi hao kutoka Shelisheli. Kiingilio cha mechi hiyo ni sh. 2,000 tu.

 Waamuzi hao ambao wanawasili saa 2.05 usiku kwa ndege ya Kenya Airways ni Allister Barra, Gerard Pool, Jean Joseph Felix Ernest na Nelson Emile Fred.

 Kamishna wa mechi hiyo Andriamiasasoa Doda Nirimboavonjy kutoka Madagascar pia anawasili leo saa 2.05 usiku kwa ndege ya Kenya Airways.

 BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Post a Comment

AddThis

 
Top