0
Muimbaji mashuhuri wa fm academia KINE MALAMU maarufu kwa jina la DIGITAL, amefariki dunia usikiuwa huu katika hospiatal ya Muhimbili alikokuwa amelaza akipatiwa matibabu

Digital alikuwa ni mwanamuziki mzuri,mpole,mwenye sauti ya juu ambayo wanamuziki wengi hawawezi kuifikia na vile vile ni mwanamuziki aliyekuwa hapendi majungu

Kutokana na tukio hili kuwa ghafla imepelekea viongozi wa fma academia kushindwa kupatikana kwa haraka na kuzungumzia msiba huu uliyoacha simanzi kwa kwao,kwamashabiki wa fm academia na mwandishi wa blog hii

enzi za uhai wake ameimba kwa uzuri sana maneno ya mungu na kuiasa jamii kutenda yaliyo mema zaidi namnukuu hapa Digital akiimba
NDUGU ZANGU TUBADILISHE TABIA ALIYOTUFANYIA MALIPO NI HAPA HAPA DUNIANI TUMWOGOPE MUNGU HATA MAANDIKO IMEANDIKA haya ni mashairi ya marehemu Digitala katika wimbo wa Fataki unaopatikana katika album mpya ya fm academia inayokwenda kwa jin ala chuki ya nini
Eee Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema umetoa na umetwaa mpuzishe kwa amani kipenzi cha Watanzania Kine Malamu Digital  AAMINA.
TAZAMA VIDEO HII KATIKA DAKIKA YA 15:NA SEKUNDE 55 UTAMUONA DGITAL AKIIMBA VEMA


Post a Comment

AddThis

 
Top