0

Shoo kabambe yaandaliwa Mwezi Ujao Jijini KINSHASA na Mkongwe wa Wanamuziki wote Inchini CONGO MZEE JEANNOT  BOMBENGA.

Madhumuni ya SHOO hiyo, nikuwashukuru na kuwaaga Mashabiki ambao walimsapoti katika kipindi cha takriban Miaka 50 ya kazi ya Muziki.
MZEE JEANNOT BOMBENGA ni mmoja kati ya Wanamuziki walio jiwekea sifa yaupekee na wenye Jina ambalo halihitaji kutambulishwa Inchini CONGO.

Huwezi kuongelea Miaka 50 yakazi ya Muziki ya Mzee JEANNOT BOMBENGA kutokana na utunzi wa Nyimbo pekee, bali ni Historia kamili ya mapenzi kati yake na Mashabiki walio mfwatilia kizazi hadi kizazi
Kutokana na Kazi yake ya Muziki, JEANNOT BOMBENGA ni Mmoja kati ya Watunzi wazuri wanao julikana Inchini CONGO. Baadhi ya Nyimbo zake hadi leo zaendelea kupendwa : ” LOLO WA NGAI, SIMONE, BOPESA YE LITEYA, ALADJI BABA, MADO, MOBALI YA MBUNKE, NALUKO YO TROP ELODIE … yaani Nyimbo alizozitunga ni Nyingi saana
sifa hizo zilipelekea atunukiwe Tuzo la ” National award of merit for culture and the arts ” Kutoka mikononi mwa WIZIRI anae husika na Mambo ya Utamaduni na Sanaa.
MZEE JEANNOT BOMBENGA kasema aliemfunza kabisa kazi ya Muziki ni  ” KABASELE JOSEPH LE GRAND KALLE “.ambae kamhimiza ajiunge na Orchestra ” AFRICAN JAZZ ” Group waliopitia Wajuzi wa Muziki , tutawataja  ROCHEREAU TABU LEY,DOKTA NICO KASANDA, VICKY LONGOMBA, EDO CLARY LUTULA, MANOU DIBANGO …
Ilipofikia Mwaka 1962, Kaunda Group lake mwenye ” VOX AFRICA ” Orchestra iliomfanya ” SAM MANGWANA ” afahamike…
MZEE JEANNOT BOMBENGA kazaliwa Mwaka 1934.

Post a Comment

AddThis

 
Top