0
Polisi nchini Japan imemfungulia mashtaka mwanamke mmoja baada ya kuona moto ukiunguza nyumba yake huku akishuhudia na kushindwa kutoa taarifa kwa jeshi la Zimamoto pamoja na watu waliokuwemo ndani.
Sababu za mwanamke huyo mwenye miaka 36  kuamua kukaa kimya alijitetea kuwa alikua akipenda kuona jinsi moto huo ulivyokua ukiwaka na hakujali thamani ya vitu vyake vilivyokua ndani ya nyumba hiyo.
Mwanamke huyo alikua akiishi floo ya kwanza ya jengo hilo katika mji wa Kagoshima pamoja na watoto wake wawili wa kike pamoja na mama yake mzazi.

Aliripotiwa kuwa licha ya kuuona moto huo hakufanya lolote na kuanza kuushangaa ulivyokua unasambaa ndani ya nyumba hiyo mpaka watoto wake waliposikia harufu ya moto wakiwa wamelala na kukimbia kwenda kumwamsha bibi yao mwenye miaka 70,lakini jitihada zao hazikufanikiwa baada ya bibi huyo kuchelewa kuamka na wao kuamua kukimbia nje na kumwacha akiteketea.
Polisi waliamua mshtaki mwanamke huyo kwa kosa la kukusuadia lakini alikiri amekosea lakini alisema alikua anapenda kuona moto ulivyokua ukiwaka.

Post a Comment

AddThis

 
Top