0





Mathias Lyamunda mwenyekiti wa asasi ya kiraia BANGONET wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma


Imeelezwa kuwa Wilaya ya Bahi ina changamoto kubwa ya kielimu kwa wanafunzi wanohitimu kutofanya vizuri

Hayo yameelezwa leo na Mathias Lyamunda mwenyekiti wa asasi ya kiraia BANGONET wilaya ya Bahi iliyopo Mkoani Dodoma pindi alipofika radio mwangaza fm wakati akielekea kwenye mahafali ya darasa la saba ya shule ya msingi Makanda

Bwana Lyamunda amesema kuwa,wilaya ya bahi haikufanya vizuri katika matokeo yaliyopita hasa kwa shule za sekondary ambapo kiwango cha ufaulu hakikuwa kizuri

Akifafanua viwango hivyo vya ufaulu bwana Lyamunda amsema waliyopata division 3 ni watano,division 4 zaidi ya 100 na divison 0 zaidi ya 500

Kutokana na matokeo hayo amewaasa wazazi Wilayani Bahi kuzingatia swala la elimu bila kujali jinsia ya watoto

......mwisho..........

Post a Comment

AddThis

 
Top