0
Kuna wakati ukitajiwa tu jina la mchekeshaji, unajikuta unacheka hata kama hujaambiwa ni kioja kipi amekifanya.
Basketmouth ni mmoja ya wachekeshaji ambao wanafahamika sana, safari hii aliongozana na mkewe kwenye show aliyokuwa akiifanya wakati wa utoaji tuzo za Headies, Nigeria.

Jamaa akaanza kuyatoa sasa kama kawaida yake; “… ndoa sio kitu rahisi ila najitahidi sana kutimiza wajibu wangu.. Kutokana  na jinsi kazi yangu ilivyo mara nyingi nakuwa sipo nyumbani, kuna wakati wiki kadhaa zinapita siko nyumbani, nikirudi tuu najitahidi kuwa karibu na familia hasa mke wangu… Natoka nae kwenye events, shopping, angalau ajione special… Nikiwa nyumbani nakuwa houseboy, nafanya kazi zote, kuwaogesha watoto, kufanya usafi, napika, nafua… nafanya kazi zote za ndani…“– Basketmouth.
Unaweza enjoy moja ya show kali za jamaa huyo kwenye video hii.

Post a Comment

AddThis

 
Top