0
Kocha Mkuu wa Mwadui ya Shinyanga, Jamhuri Kihwelo amesema kipigo cha bao 1-0 walichokipata kutoka kwa Toto African si mwisho wa safari.

Katika mechi hiyo ya Ligi Daraja la Kwanza iliyopigwa leo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini hapa, bao pekee la wenyeji lilifungwa na Andusi Issa katika dakika ya 78.
Andus aliwatoka mabeki wa Mwadui kabla ya kugeuka na kupiga mkwaju mkali kutoka mita 22, ukajaa wavuni.
“Utaona mechi hii ilikuwa yetu, tumepoteza nafasi nyingi na tulikuwa na nafasi ya kushinda.

“Lakini huu si mwisho wa safari, bado tuna njia ya kupita na kufanya vizuri zaidi,” alisema Julio.
Mechi nyingine ya Ligi Daraja la Kwanza iliyochezwa leo jijini Dar es Salaam, Friends Rangers ya Magomeni Kagera iliitungua Lipuli kwa mabao 2-1.

Post a Comment

AddThis

 
Top