0
                       Dada Anakonda (jay dee) na De Caprio (Fally Ipupa)



Ukitaka kujua ugumu ama urahisi wa kumiliki bendi muulize Muumin Mwinyijuma atakwambia na Tamtam yake, Muulize Asha Baraka na Twanga yake, Muulize Engineer Martin Kasyanju na Ngwasuma yake ama Muulize Ally Choki na Extra Bongo yake.

Lady Jaydee aka Binti Machozi ni mwanamuziki ambaye kama ni kuchora chati ya mafanikio utaona inaanzia chini kabisa na ikienda ikiongezeka kila uchao, tangu amemiliki bendi kuna mara kadhaa amejaribu kuhujumiwa bila mafanikio na anazidi kusonga tuu.

Pichani akiwa jijini Nairobi na Mwanamuziki Mahiri Fally Ipupa De Caprio ambaye naye anapasua anga si tu la Africa bali duniani, hii ilikuwa jijini Nairobi, ilikuwa kitu gani? Je wana program pamoja? tega sikio hapa hapa utapata jibu lako. 


Post a Comment

AddThis

 
Top