0

KOPUNOVIC AKIHOJIWA NA WAANDISHI WA GAZETI LA CHAMPIONI.

Kocha mpya wa Simba, Goran Kopunovic ametangaza mapemaa kwa wachezaji kuwa wajue yeye si mtu wa mzaha katika suala la nidhamu.
Kopunovic amesema angependa kufanya vizuri na anategemea ushirikiano wa karibu kwa wachezaji, benchi la ufundi, uongozi na wanachama na mashabiki.

Lakini akasisitiza, suala la nidhamu litakuwa namba moja na hatakuwa na mzaha.

“Hakuna kitu kinafanyika kwa ufasaha katika maisha ya mwanadamu kama nidhamu haina uhakika.
“Hili ni sehemu ya misingi bora ya kazi, itakuwa ni muhimu lipewe kipaumbele ni suala muhimu,” alisema.

Rais huyo wa Serbia ametua kuchukua nafasi ya Patrick Phiri baada ya kuingoza Simba katika mechi nane za Ligi Kuu Bara akiwa ameshinda moja, sare sita na kupoteza moja.

Post a Comment

AddThis

 
Top