Hii ndiyo kauli ya Staa huyu wa filamu za Nigeria kwa mashabiki wake kuhusu talaka toka kwa mume wake
Kumekuwepo na maneno mengi baada ya staa wa Filamu wa Nigeria Ini Edo kutengana na mume wake Philip Ehiagniwa.
Lakini mwenyewe amefunguka na kusema mashabiki wake wala waandishi wa habari hawapaswi kuzungumzia talaka yake kwa kuwa ni mambo binafsi huku yeye akitumia muda wake mwingi kufanya mambo yake mwenyewe.
“Nataka watu watulie na kufanya mambo yao badala ya kunizungumzia kuhusu talaka yangu,na siwezi kuzungumzia lolote kuhusiana na hilo,ni mambo yaliyopita na tuyaache kama yalivyo,mimi sijali.
Kwa sasa kuna taarifa kuwa baada ya kutengana mume wake yuko katika mahusiano na mwanamke kutoka nchini Ghana.
Post a Comment