0
Mkurungezi wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ Asha Baraka amemuonya msanii anayefanya vizuri kwenye muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kutojaribu kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulevya na kusema akijaribu atapotea.

Akizungumza na Ijumaa hivi karubini, Asha Baraka ‘Iron Lady’ alisema Diamond anaweza kufanya vizuri kwa miaka mingi inayokuja lakini akijaribu kutumia dawa hizo ataishia pabaya.
“Tumeona wasanii wengi wa Tanzania ambao awali walikuwa wanafanya vizuri lakini baada ya kujaa sifa na kukutana na marafiki wengi pamoja na makundi wakazama kwenye dawa za kulevya na sasa wanatapatapa na kubaki kulaumu wakati wenyewe wamejiharibia,” alisema Iron Lady.

Post a Comment

AddThis

 
Top