0
Sudan ndiyo timu pekee kutoka Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati iliyofanikiwa kushinda mechi yake ya kufuzu kucheza Kombe la Mataifa Afrika leo.

Sudan ikiwa imeishinda Nigeria kwa bao 1-0 lililofungwa na Bebeker katika dakika ya 42.
Lakini timu nyingine za ukanda huu, ethiopia na Uganda zote zimepoteza tena zikiwa nyumbani.
Ethiopia imepigwa bao 2-0 na Mali wakati Uganda imechapwa 1-0 na Togo.
Mechi nyingine ya jirani wa Tanzania Malawi, wakiwa nyumbani nao wamekiona cha moto kwa kuchapwa kwa mabao 2-0 na Algeria.

Post a Comment

AddThis

 
Top