0
Vituko vya Wachungaji wanaotajwa kuwa ‘feki’ huko Kenya vimekua vingi kila wakati kwenye nchi hiyo huku wengine wakiingia kwenye kashfa ya kuhonga watu hela ili watoe ushuhuda wa uongo kanisani, wengine wakitajwa kujihusisha na uhusiano wa mapenzi ya jinsia moja…. hizo ni baadhi tu ya kashfa zinazowakumba. Kingine kipya ni hiki cha mchungaji mmoja huko Mshomoroni huko Mombasa Kenya walimkimbiza mchungaji huyu na waumini wake kuwaondoa eneo hilo kutokana na kile walichodai kwamba ni mambo yasiyo ya kawaida yanayofanyika kwenye kanisa lake.

Inadaiwa Mchungaji huyu ana mazoea ya kufanya mapenzi mpaka na wake za watu ambapo mashuhuda wanasema ‘pia Waumini wanakunywa pombe alafu wanadance wawiliwawili wanaambiwa shika mwenzako mahali unataka na Wanaume hapa Kanisani wameambiwa kila Mwanaume atapewa Wanawake watatu’

Mashuhuda wengine unaweza kuwasikiliza kwa kubonyeza play hapa chini…

Post a Comment

AddThis

 
Top