0
Wakali wa hiphop kutoka Mwanza (88.1 CloudsFM) Young Killer na Fid Q wameingia kwenye headlines na director Nisher ambae ni mshindi kwenye Tuzo za watu 2014 ambapo kinachofanyika ni video ya single ya Young Killer aliyomshirikisha Fid Q.
Unajua Young killer ameiambia millardayo.com mambo yapi matano?
1. Video imetengenezwa ndani ya siku moja tu 2. location ni Tegeta ndani ya sehemu moja tu ambayo ni eneo la kiwanda, 3. Ni single ambayo inazungumzia 13 ambayo ni tarehe ya kuzaliwa Fid Q (August 13) na yeye Young killer aliezaliwa April 13.
4. gharama za video Director mwenyewe amepewa Milioni 4, location imelipiwa shilingi laki 2 ukijumlisha na gharama za magari na pikipiki jumla inafikia kwenye milioni sita na nusu. 5. Pikipiki zilipangwa kutumika lakini zikaachwa, muda uliisha lakini pia Killer alishindwa kuendesha.
 picha zote hizi zimetoka kwenye page za instagram za Fid Q >>> HAPA na Nisher >>> HAPA



Post a Comment

AddThis

 
Top