mwandishi wetu/ijumaawikienda
MWIGIZAJI
wa sinema za Kibongo, Ummy Wenslaus ‘Dokii’ ameanzisha urafiki wa
karibu sana na Kocha wa Timu ya Yanga, Hans van der Pluijm, Raia wa
Uholanzi.
Ukaribu wa Dokii na kocha huyo ulichipukia kwa kasi Januari, mwaka
huu walipokutana katika Kombe la Mapinduzi, Zanzibar kisha kuzidi
kuwasiliana kwa ukaribu hadi kuwafanya wapenda ‘ubuyu’ wautilie mashaka.
Alipotafutwa Dokii ili aweze kuufafanua zaidi ukaribu wao kama
umejiongeza zaidi na kuwa wapenzi, alijibu kwa kifupi tu pasipo
kufafanua zaidi.“Hakuna tatizo mimi kuwa naye karibu, namkubali na yeye
ananikubali pia. Ni mshkaji sana jamaa.”
Kocha huyo hakupatikana hewani alipotafutwa lakini jitihada zinaendelea.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment