0


Hatimaye mwanadada Jacqueline Wolper ameamua kuweka wazi kilichotokea mpaka kuamua kubadili Dini yake ya Uislamu na kurudi kwenye ukristo tena.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii mwanadada huyu wa bongo movies ametoa ujumbe ufuatao kwa mashabiki wake. 

“…mambo mashabiki zangu.sikua na njia nyingne ya kulikwepa hili na naamini kua kwa wale mashabki zangu waislam amtomaind maana akuna mtu wakumsikiliza chini ya hanga zaidi ya wazazi so imenipasa kurudi kanisani kwa kauli ya wazazi wangu.

naamin kama haujaolewa hata uwe na miaka mingapi bado unatakiwa kua chini ya imaya ya wazazi hata ukifa ujue unazikwaje na mimi ni binadam sijui saa wala dakika.

muhm ni kuwajuza nakuwaelewesha mashabiki zangu staki maswali nawapenda wote…”

Hapo awali iliripotiwa kuwa mwanadada huyu ameamua kuwa mkristo tena baada ya penzi lake lililosababisha abadili dini na kuwa muislamu na jamaa aitwaye 'Dallas' kuvunjika hivi karibuni.

Swali ni je, atabadili dini tena akitokea mwingine wa dini aliyo tofauti na sasa?

Post a Comment

AddThis

 
Top