0
Baby Joseph Madaha ndiye ambaye wiki hii yuko hapa kujibu maswali 10 ambayo mwandishi wetu Gladness Mallya alimuuliza. Ilikuwa hivi;
 Staa Baby Joseph Madaha.
Ijumaa: Umekuwa ukitajwa kuwa wewe ni msanii wa kike unayeongoza kwa kubadilisha mabwana kila kukicha, hili likoje?
Baby Madaha: Ukweli hiyo huwa inatokea tu na huwa sipendi kusumbuliwa na mwanaume, nikiona ananizingua nammwaga. Hata hivyo, kwa sasa nimeamua kutulia kwanza, nafanya kazi, mapenzi pembeni.
Ijumaa: Unadhani kwa nini umekuwa ukiingia kwenye uhusiano kisha kutoswa, ni umachepele wako au kitu gani?
Baby Madaha: Mimi wala siyo machepele kama watu wanavyonifikiria na kiukweli huwa nawaacha mimi na siyo wao kuniacha.
Ijumaa: Mpaka sasa umeshakuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume wangapi?
Baby Madaha: Wanaume niliotembea nao ni siri yangu kwa sababu nikitaja idadi hapa watu watalia na wewe mwandishi unaweza kuzimia.
Ijumaa: Kuna tetesi kwamba wewe na msanii mwenzako Isabela Mpanda huwa mnaishi kama mke na mume, hebu eleza ukweli wa hili jambo.
Baby Madaha: Siyo kweli na sijawahi kufanya usagaji katika maisha yangu. Isabela ni rafiki yangu tunafanya kazi, hayo mengine ni maneno ya watu tu.
Ijumaa: Vipi kuhusu penzi lako na meneja wako, Joe Kariuki limeishia wapi? Mbona safari za Nairobi sasa zimepungua tofauti na zamani?
Baby Madaha: Mapenzi na Joe yameisha, kuhusu kwenda Nairobi nimepunguza kwa sababu nafanya kazi zangu za filamu. Mkataba wangu na kampuni ya Candy & Candy unaisha mwaka ujao na unaniruhusu kufanya kazi zangu za filamu, wao nafanya nao muziki tu.

Post a Comment

AddThis

 
Top