0
BENO NJOVU (KULIA) WAKATI AKIWA YANGA, KULIA NI MWENYEKITI WA YANGA, YUSUF MANJI.

Yanga imemuajiri Daktari Jonas Tiboroha kuchukua nafasi ya aliyekuwa Katibu Mkuu, Beno Njovu.

Njovu ameondoka Yanga baada ya mkataba wake kwisha na amekuwa akiendelea na shughuli zake mbalimbali kwa kuwa alihitaji muda zaidi.

Ili kuziba nafasi yake, taarifa za uhakika zinaeleza Dk Tiboroha ni mhadhiri kwenye vyuo vikuu mbalimbali vya ndani na nje ya Tanzania.


Imeelezwa daktari huyo amewahi kufanya kazi Norway na Sweden ambako pia alipata elimu yake kwa kiwango cha Masters na baadaye PhD.

Post a Comment

AddThis

 
Top