0



Katika mahojiano yake na Waandishi wa Habari, Mama ” HALIMA “, ambae ndie Mke Halali wa BABIA NDONGA kajieleza kwa kirefu kutokana na Kifo cha Mmewe.
HALIMA : Ilitokea Siku Moja BABIA kaniambia, ” Sikiliza HALIMA, Sikutaki tena, Tokea leo hii jisikie kuwa huru, jitegemee mwenyewe. Nimeshampata Kimwana mwengine ” ( yasemekana Kimwana huyo ni  Binti wa Waziri Mmoja kwenye Serekali ya Congo ).
Nikamwambia, hebu Mme wangu, kweli waweza kuniacha Baada ya takriban miaka Minane ya Ndoa, nakwenda kuishi na Mwanamke mwengine? Maneno hayo yaliniuzi sana, Nikafungasha vitu vyangu na kuondoka Nyumbani pale ambapo tulikua tukiishi pamoja. nikahamia sehemu nyingine. Ila tukawa tunaendelea kuwasiliana kupitia njia ya Simu.
Mimi HALIMA ndie Mama mlezi wa Watoto wa BABIA alio wazaa Inje na Wanawake wengine. Hadi leo Wako Nyumbani kwetu KINSHASA kwenye Barabara ya FUNA. Watoto wake PRINCE na ANNA wanaishi kwetu.
SIKU ALIO FARIKI BABIA, KWAKWELI ALIKUA NYUMBANI KWANGU, Mimi ndo nimemuitisha aje tuzungumze. Ila kabla yakuja Nyumbani kwangu, katokea Uwanja wa Ndege akimsubiria Kimada wake aliekua akitokea Ulaya, kwa Bahati mbaya, Mwanamke huyo hajatokea, yaani kahairisha Safari yake bila kumpa BABIA taarifa yeyote.
BABIA kaja Nyumbani kwangu, Kabisha hodi mlangoni, Nilikua niko kwenye Msala nikipiga Rakaa, Mkononi mwangu nilikua nikishikilia Tasbihi, kwakua Mimi ni Muislamu.
Nikaenda kumfungulia BABIA Mlango, pindi tuu alipo ingia ndani nakukaa kwenye Kiti, BABIA akesema HALIMA nahitaji Mazungumzo yakina na!!! kabla hata hajamalizia maneno, Akawa anashindwa kabisa kuendelea kuongea, huku nikamuona Mtu akiwa mwenye kupooza Mikono hadi kwenye Miguu.
Nikashtushwa na hali hiyo, Mwenyewe nikaanza kupiga kelele,  BABIA NIKITU GANI, UNAUMWA NINI, NIKAOMBA MSAADA KWA MAJIRANI, WAKAJA, TUKAMUWAHISHA KWA HARAKA KWENYE HOSPITALI NDOGO KWA DOKTA JUDE.
MTANGAZAJI : Kwani ilichukua Mda gani tokea pale mlivyo achana? yeye akiwa anaishi Nyumbani kwake na wewe Ukawa unapanga Sehemu yako ?
HALIMA : Ilichukua kama Wiki Moja na Siku Tano vile tokea tuachane. Mwenyewe ndo kaniacha, Kaniambia fungasha vitu vyako, anza Maisha yako jinsi uonavyo. Bado ninayo MSG yake nyingi tuu aliokua akinitumia kupitia mtandao wa VIBER. kasema HALIMA JITEGEMEE MWENYEWE, ACHANA NAMIMI, NINAYO MIPANGO MINGI SANA AKILINI MWANGU. MWAKA HUU NILAZIMA NIENDE ZANGU ULAYA, NIMESHA KAA SIKU ZA KUTOSHA JIJINI ” LUANDA “, WAKATI WAWADIA SASA KWAMIMI KUMALIZIA ALBUM YANGU.
Haya narudilia ongezi la hapo awali, TULIPO MFIKISHA BABIA KWENYE HOSPITALI YA DOKTA JUDE, YEYE KAMPOKEA, kamchunguza na kumchoma sindano, Ndipo katushauri tumpeleke kwenye Hospitali kubwa, hali yake yahitaji Tiba nzito zaidi. Ilibidi tumkimbizie kwenye Hospitali KUU, Wakampokea na kumpeleka Moja kwa Moja kwenye Chumba cha dharura, wakamuweka Chupa za maji kwa haraka sana. Ila hali ya BABIA ilikua si nzuri kabisa, alikua hana tena Kauli, kawa Mtu mwenye kutizama tuu.
Nikachukua Simu yake, Nikaanza kuwapigia Marafiki zake nakuwajulisha hali halisi alionayo BABIA, Hakuna yeyote alie jitokeza na kuja kumjulia hali mwenzao. Kutokana na hali yangu ya uchovu, Ma Dokta wakanishauri niende Inje maramoja wao wanaendelea na kazi ya kumuhudumia.
BAADA YA MDA, NIKAAMUA KURUDI CHUMBANI KUCHUNGUZA HALI YA BABIA INAENDELEAJE ?, NDIPO MA DOKTA WAKANIAMBIA KWAMBA BABIA KAFARIKI DUNIA. (ANALIA …)
MTANGAZAJI : Kwani Wewe na huyo Mwanamke mwengine Mmshawahi kuonana ? Mmegombana kiukewenza? au kubadirishana maneno kwenye Simu?
HALIMA : Kuna Siku kanitumia Ujumbe kupitia MSG ya Facebook, kanitukana, kasema BABIA ni wakwake, anajiandaa kuja kumchukua na kuondoka naye, Mimi simuwezi , Baba yake ni KIGOGO kwenye Serekali ya CONGO. Hakuna kitakacho mzuia asifunge Ndoa na BABIA. kasema Mimi ni mjinga. Wala sijawahi kumuona , hata BABIA mwenyewe alikua bado hajamuona. Leo hii ndo nimepata taarifa kwamba kawasili JIJINI LUANDA.
MTANGAZAJI : HEBU TUAMBIE UKWELI Kuhusu Safari yako ya kwenda kwenye MJI WA WAMBO, Ulienda huko kufanya nini  ?
HALIMA : Kwenye MJI WA WAMBO nilienda kufanya BIASHARA ZANGU, hua nauza CD, BABIA alivyosikia niko WAMBO, kanifwata kwa haraka sana, kajakunitishia Nirudi haraka LUANDA, vinginevyo atanifanyia mpango nipelekwe moja kwa moja CONGO KINSHASA.
Nikamuambia kamwe haitowezekana kwangu mimi nirudi CONGO, Mwanaume gani wewe usie nijali? sipati hata Dola 10 kutoka kwako. Ukwali ni kwamba BABIA kaambiwa na Watu kanakwamba Mimi nimeolewa WANDO ndo kwamaana hiyo kaja akiwa mwenye hasira sana. kanigombeza hadi tukaishia Polisi.
Bado tukiwa kwenye MJI WA WAMBO, BABIA kamleta nakunionyesha Mwanamke mwengine Mbele ya macho yangu,  Dada huyo anajulikana kwa Jina la ” LOTTY “, BABIA kanifahamisha ya kwamba huyo ndo Mkewe tokea sasa. Nikamwambia BABIA naomba unipe talaka, nimesha choshwa na vituko vyako. Kwani amenisikia ?
Nikaamua kumuacha pale kwenye MJI WA WAMBO nikarudi zangu LUANDA, Bado akiwa WAMBO, BABIA kapata tenda ya kufanya SHOO mbili. Alipopewa taarifa kwamba nimeshakimbilia LUANDA, Huyo kafunga Safari nakunifwata hadi LUANDA, kaja kuniomba Msamaha, kanitaka radhi, kasema Mimi ndie MAMA WATOTO WAKE, kapagawishwa na Mambo ya Ulimwengu. Kanigea Zawadi ya Dola Elfu Tatu, na Mkufu wa Dhahabu. BABIA kaangua kilio … Moyo wa Umama,Moyo wa Huruma ukanijia, nikamsamehe… Tukaendelea kuishi tena pamoja.
MTANGAZAJI : Tumesikia kwamba Zawadi hiyo ya Mkufu wa DHAHABU ilileta kasheshe iliompelekea BABIA kuwekwa Mbaroni Polisi, ilikuaje?
HALIMA : Kumbe Mkufu huo wa Dhahabu, BABIA kapewa na Kimada wake LOTTY, walipo pezana zawadi zao kutokana na Mapenzi yao mimi wala sikuwepo. Yasemekana  BABIA alikua kampa LOTTY ahadi za uongo kama ndie Mchumba wake, wataishia kufunga Ndoa. Hali hiyo ya Wachumba, ikamfanya LOTTY aanze kumgharamia BABIA kwakumnunulia vitu kadha, ikiwemo Mkufu huo.
Ikatokea Siku moja, BABIA kapokea simu, alie mpigia ni LOTTY, wakaanza kujibishana kwa ukali, nikamsikia LOTTY akisema UMENISALITI, UMEMRUDILIA HALIMA, HAKUNA SHIDA, MWENYEWE UTAONA YATAKAYO KUKUTA.
Wala haijapita Siku, LOTTY huyo katua kwenye MJI WA LUANDA, akiongozana na MABAUNSA wawili waliojaa sawasawa. Jamaa hao walimshikilia BABIA, WAKMTWANGA MBAYA SANA, hadi kaumia Usoni, Mdomo ukamjaa kwelikweli.
Polisi wakaja kuingili kati, wakawachukua wote nakuwapeleka Kituoni kuwasikiliza. Wamewekwa huko kwa siku mbili mfululizo. Mimi nikaambiwa nirudi zangu Nyumbani wala sina hatia yeyote. Kesi yawahusu Wapenzi, Huko waliko kabidhiana Zawadi zao wala mimi sikuwepo.
Huko Kituoni cha Polisi, Muafaka ulipatikana, BABIA KAKUBALI DENI, KASAINI KARATASI NA KATOA AHADI YA KUMRUDISHIA LOTTY VITU VYAKE.
JAMANI ACHENI KUNIPAKAZIA, WALA SIO MIMI NILIE MUUWA BABIA, ALIKUA TAYARI KESHA NIKATAA, KASEMA HALIMA BASI SIKUTAKI TENA, KWENYE MAISHA YANGU, NIMESHA MPATA ” HELENA MWANZA “. YEYE KANIPA AHADI YAKUNISAIDIA NA KUNIPELEKA ULAYA NIKAMALIZIE ALBUM YANGU. JAMANI ,NTAMUUAJE BABA WATOTO WANGU? SIWEZI KUMTAKIA BABIA UBAYA WOWOTE. ACHENI KUNICHAFUA!!!
NDIO BABIA ALIKUA MME WANGU, NDIE PIA KANILEA KWAHIYO KWA UPANDE MWENGINE NILIKUA NIKIMCHUKULIA KAMA BABA YANGU. WALA SIJAMUUWA BABIA, KAFA KIFO CHA KAWAIDA KUTOKANA NA MAPENZI YAKE MUNGU. NILIVYO HAPA MWENYEWE NASHINDWA KABISA KUAMIN

Post a Comment

AddThis

 
Top