0
Stori: Gladness Mallya na Hamida Hassan

Miss Sinza aliyeshiriki Miss Tanzania 2011, Husna Maulid amekanyaga skendo ya wizi baada ya kudaiwa kuwahi ‘kumdokolea’ aliyekuwa mpenzi wake, Mwani Rajabu ‘Mkongo’.
 Miss Sinza aliyeshiriki Miss Tanzania 2011, Husna Maulid.

Chanzo kilichoomba hifadhi ya jina lake kilidai kuwa, kutokana na tabia hiyo Husna alitoswa na mpenzi wake huyo ambaye ni raia wa Kongo.Baada ya kuzinyaka habari hizo mapaparazi wetu walimtafuta Mwani ambaye yupo Bongo kwa sasa na alipopatikana alisema:
“Yaani Husna hana kasoro nyingine zaidi ya hiyo kwani amekuwa akinifanyia hivyo tunapokuwa hotelini, sasa tabia yake ilinichosha nikaamua kuachana naye.”
Kwa upande wake Husna alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo alikanusha vikali na kusema hajawahi kuwa mwizi bali anazushiwa.
“Mimi siyo mwizi na sijawahi, naomba muulize vizuri huyo Mkongo kama nilishawahi kumuibia nini,” alisema Husna.

Post a Comment

AddThis

 
Top