0
SIKU chache baada muigizaji nyota wa filamu nchini, Rose Ndauka kutemana na bwana wake, Malik Bandawe, Jumanne iliyopita aliangusha bonge la sherehe iliyofana ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Collosseum, iliyopo Kariakoo jijini Dar na kuhudhuriwa na mastaa kibao, Ijumaa lilikuwepo.
 Msanii nyota wa filamu nchini, Jack wa Chuz (kushoto) akimtunza msanii mwenzake, Rose Ndauka (kulia)
Sherehe hiyo ya Rose, ambaye alizaliwa siku moja na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ilishuhudia mastaa wengi wa kike walioalikwa, licha ya kunywa na kula kwa kadiri walivyojisikia, lakini pia wakiwa wamevalia vivazi vilivyoonyesha sehemu kubwa ya miili yao.
 Msanii wa filamu nchini, Mayasa (kushoto) akitoa sapoti ya kufungua shampeni katika sherehe hiyo ya bethidei ya Rose Ndauka.
Katika pati hiyo kulikuwa na vinywaji vyenye kilevi na visivyo na kilevi, huku pia vyakula vya aina mbalimbali vikipatikana, kiasi kwamba hadi gazeti hili linaondoka, pombe na vyakula bado vilikuwepo.
Lakini kivutio zaidi kwenye shughuli hiyo iliyoshuhudia pia Mussa Issa ‘Cloud’ anayekaimu uongozi wa Bongo Movie Unity akiutangaza upya umoja wao, alikuwa ni shoga mkubwa wa Rose, Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuzi’ambaye alionekana ‘akimkogesha’ fedha rafikiye wakati wa kutoa zawadi ulipowadia.
 Msanii nyota wa filamu Bongo, Shamsa Ford naye pia alikuwepo.
Akiwa kwenye sherehe hiyo, Rose alionekana kuwa mwenye furaha tofauti na siku chache zilizopita baada ya kukosana na mchumba wake huyo. Katika zoezi la vinywaji, baadhi ya waalikwa walikunywa hadi kulewa chakari na hivyo kuleta burudani nyingine.
 Msanii nyota wa filamu Bongo, Shamsa Ford naye pia alikuwepo.
Akiwa kwenye sherehe hiyo, Rose alionekana kuwa mwenye furaha tofauti na siku chache zilizopita baada ya kukosana na mchumba wake huyo. Katika zoezi la vinywaji, baadhi ya waalikwa walikunywa hadi kulewa chakari na hivyo kuleta burudani nyingine.

Post a Comment

AddThis

 
Top